Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu kiongozi Mhandisi Zena Ahmed Said, akiongoza kikao kazi cha kupitia sera ya mageuzi ya  kimkakati katika  sekta ya Utalii zanzibar

Yasemwa hayo leo Hoteli ya Golden Tulip Uwanja wa Ndege : upitishwaji wa sera mpya  itasaidia kuondoa changamoto zilizokuwepo hapo awali kwa  kuanzisha vyuo vya kutoa elimu kuhusiana na Utalii ili kuongeza Pato la Taifa


Aidha Katibu Mkuu Wizara ya Utalii na Mambo ya Kale  Abuod Suleiman Jumbe amefahamisha kuwa  imefanya KAZI kubwa ya kuichambua sera iliyopo awali na  kuangalia mapungufu na changammoto zilizomo ili kurekebisha changamoto hizo na sekta ya utalii izidi kukuwa kama raisi wa zanzibar anavyotaka.


Aidha amefahamisha kuwa sera hiyo itaweza kusaidia kukuza zaidi kwa soko letu la utalii na serikali kupata mapato ya asilimia 80.5 na pamoja kupata kipato kwa mtu binafsi

Aidha amefahamisha kutokana na mageuzi hayo ya  kimkakati imepelekea kuifungua Pemba kiutalii na kujitokeza kwa wawekezaji  mbalimbali  kuunga mkono juhudi hiyo  kwa kuzingatia maadili ya kizanzibari
.

 Nao Washiriki wa kikao hicho wamesema kuwa sera hiyo  itapewa kipaombele kwa  wananchi kwani bila Elimu utalii utaporomoka na kupata kesi zisizozamsingi na jamii kukosa maendeleo .